Psalms 103:1-6
Upendo Wa Mungu
(Zaburi Ya Daudi)
1 aEe nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
2 bEe nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,
3 cakusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,
4 daukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji ya upendo na huruma,
5 eatosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema,
ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
6 f Bwana hutenda haki,
naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
Copyright information for
SwhKC