Psalms 103:1-6

Upendo Wa Mungu

(Zaburi Ya Daudi)


1 aEe nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.

2 bEe nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,

3 cakusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,

4 daukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji ya upendo na huruma,

5 eatosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema,
ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.


6 f Bwana hutenda haki,
naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.

Copyright information for SwhKC